

TQ: Ni kitu gani kilichokufanya udumu kwenye ndoa yako mpaka sasa jambo ambalo wasanii wengi linawashinda?Sandra: Unajua mwanamke mjinga anaivunja ndoa yake mwenyewe, mimi siyo mjinga hivyo nailinda kwa kadiri ninavyoweza. Uvumilivu, kupendana kwa dhati na kuheshimiana ndiyo siri kubwa.
TQ: Unapokuwa nyumbani kwako huwa unapendelea kuvaa mavazi ya aina gani, hususan ukiwa chumbani na mumeo?Sandra: Nikiwa nyumbani kwa kuwa naishi na wanangu huwa napenda kujifunga kanga na kuvaa madira lakini nikiwa chumbani, huko ni full kujiachia.
TQ: Inadaiwa wewe ni kati ya mastaa wasiopenda kufanya kazi za nyumbani na mara nyingi unamuachia majukumu hausigeli ikiwemo kumpikia mumeo, hili likoje?
Sandra: Sipendi kabisa mume wangu apikiwe chakula na hausigeli, mimi ni mwanamke ninayejua majukumu yangu, kwa hiyo hausigeli huwa ananisaidia tu.
TQ: Hivi siku ikitokea umemfumania mumeo utafanyaje?
Sandra: Kwa kweli naomba Mungu hilo lisitokee maana sijui maumivu nitakayoyapata, kwanza nitamsamehe sababu nampenda sana mume wangu.
TQ: Umeshawahi kuchepuka? Kuwa mkweli Sandra.
Sandra: Sijawahi kufanya hicho kitu wala sifikirii. Nifuate nini wakati kila kitu nakipata kwa mume wangu jamani? Sina tamaa za kijinga mimi.TQ: Hili la wasanii kuibiana mabwana halikutii hofu?
Sandra: Mimi sihofii hilo kabisa maana najiamini mno, kama mtu ni m****** malaya tu hata umchunge vipi akiwataka atatembea nao.
TQ: Ni sehemu gani ambayo inakupa mzuka zaidi kwenye jumba la mahaba?
Sandra: Ninapokuwa hayo maeneo kila kona ya mwili wangu huwa imejaa msisimko, ila napendelea zaidi ‘romance’.TQ: Siku za wikiendi unapendelea kufanya nini?
Sandra: Napenda kutoka na familia yangu kwenda ufukweni kuogelea na kubadilishana mawazo na mume wangu. TQ: Utapenda watoto wako warithi fani yako ya uigizaji?
Sandra: Sifikirii wanangu waje kuwa wasanii, kikubwa nawaombea mafanikio wawe watu bora zaidi kwenye taifa.TQ: Hivi baada ya kuolewa kwenda viwanja ndo’ basi?
Sandra: Naiheshimu sana ndoa yangu, sioni sababu ya kwenda kukesha klabu, huwa napenda kutulia chumbani na mume wangu na kutazama muvi.
No comments:
Post a Comment