
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeshinda kesi dhidi ya aliyekuwa mwanachama wake Zitto Kabwe.
Katika hukumu hiyo iliyotolewa leo na Jaji Mziray,Mahakama imewaruhusu CHADEMA kuendelea na taratibu zake za Awali. Aidha, Mahakama imeamuru Zitto Kabwe alipe gharama zote za kesi.
Ikumbukwe kuwa, mwaka jana Zitto Kabwe aliweka pingamizi mahakamani kuzuia kikao cha Kamati Kuu ya chama hicho kumjadili mpaka pale shauri lake litakaposikilizwa na Baraza Kuu la Chama hicho.
0 comments:
Post a Comment