

Miongoni mwa mastaa hao ni mwanamuziki Davido Adeleke, aliyekuwa na shoo kwenye tamasha moja nchini Kenya hivyo hakuweza kupiga kura.

Mwanamuziki mwingine Flavour N'abania yeye alikuwa jijini London kwenye Tamasha la Dance Afrique. Huku mastaa wengine wakiwemo Tiwa Savage na P Square wakihudhuria tamasha hilo.

Mtangazaji Toke Makinwa yeye alikuwa nchini China wakati wa tukio hilo.
Mwanamuziki Wizkid ni staa mwingine ambaye hakupiga kura kutokana na shoo yake aliyokuwa nayo huko Dubai.

Matokeo ya uchaguzi huo yanatarajiwa kutangazwa leo jioni ambapo Rais Goodluck Jonathan wa chama tawala cha PDP na Muhammud Buhari kutoka chama cha upinzani cha APC wanachuana vikali.
0 comments:
Post a Comment