Abdulrahman Hamis Clemensi enzi za uhai wake.JESHI la Polisi Mkoa wa Morogoro linamshikilia Zamili Shabani kwa madai ya kumnyonga hadi kumuua mtoto wake wa kambo, (mwaka mmoja na nusu) huku mauaji hayo yakihusishwa na wivu wa mapenzi.
“Mwanzoni mwa mwaka huu alifika Zamili akitokea Zanzibar. Kwa taarifa tulizonazo Zamili alikuwa na ishu kubwa kule ndiyo maana akaamua kuja huku. “Unajua vijijini, mtu akitokea mjini wanawake wanamshobokea. Dada yetu Rehema akadanganywa na Zamili akatoka kwenye ndoa yake na kuolewa naye mwezi wa saba mwaka huu.
0 comments:
Post a Comment