KIKUNDI cha akina mama wa Ujirani Mwema Mbezi jana walitembelea kituo cha watoto yatima cha Alfurqan Islamic Centre kilichopo Chanika jijini Dar es Salaam.
Kinamama hao wakiongozwa na mwenyekiti wao, Rose Kanijo, walitoa msaada wa vitu mbalimbali vikiwemo vyakula, nguo na viatu vya watoto.
Mbali na msaada huo wanakikundi hao walipika chakula cha mchana na kujumuika na watoto wapatao hamsini ambao walikula nao. Pia walikata keki za baadhi ya watoto na wanachama waliokuwa wakiadhimisha siku zao za kuzaliwa.
Baada ya kisherehe hicho kidogo mlezi wa watoto hao, Athumani Sultani, alitoa shukrani zake kwa akina mama hao kwa kuwakumbuka watoto hao ambao wamekuwa wakihitaji misaada mbalimbali kutokana hali yao.
0 comments:
Post a Comment