2015-02-11

MAMBO HAYO BAADHI YA WAFANYABIASHARA JIJINI DAR WAFUNGA MADUKA KUMUUNGA MKONO MWENYEKITI WAO


Baadhi ya maduka Mtaa wa Gerezani, Kariakoo yakiwa yamefungwa leo.

Mbali na maduka mengine kufungwa, baadhi ya maduka yalikuwa wazi yakiendelea kutoa huduma kwa wateja.

Baadhi ya wafanyabiashara wa maduka Mtaa wa Gerezani, Kariakoo jijini Dar es Salaam leo wamegoma kufungua maduka yao huku wengine wakiwa wamefungua maduka na kuendelea na biashara.

Wafanyabiashara hao wameamua kufunga maduka kwa kile kinachodaiwa kumuunga mkono Mwenyekiti wao, Johnson Minja (34), anayepandishwa kizimbani leo katika Mahakama ya Mkoa wa Dodoma kwa makosa mawili likiwamo la kuzuia ukusanyaji wa kodi kwa kutumia mashine za kielektroniki (EFDs).

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...