2015-02-11

Ni balaaaaaa:Ngassa amwaga mboga je, wajua ni mboga gani?..bofya hapa kuona aina ya mboga hiyo!!!!!!!!!!!!!!!!



Mchezaji wa Yanga Mrisho Ngassa (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano iliofanyika jana.

Ngassa au ‘Uncle’ kama anavyofahamika kwa mashabiki wa klabu hiyo alieleza kuwa, hataki tena kucheza soka nchini baada ya mkataba wake na Yanga kumalizika msimu huu.

Winga wa Yanga, Mrisho Ngassa ni kama amemwaga mboga kwenye klabu hiyo baada ya jana kuiumbua akibainisha masaibu mbalimbali yaliyomfika tangu arejee klabuni hapo akitokea Azam na Simba. 



Je,unahitaji kufahamu visa:soma hapa

Ni sheeeeeda!!! Ommy Dimpoz: Inzi Kufa Kwenye Kidonda Sio Ufala....je wajua kwa nini amesema hivyo soma hapa kuona kisa!!!!!!!!!!!!!!!!!


Ngassa au ‘Uncle’ kama anavyofahamika kwa mashabiki wa klabu hiyo alieleza kuwa, hataki tena kucheza soka nchini baada ya mkataba wake na Yanga kumalizika msimu huu.

Alibainisha mbele ya waandishi wa habari kuwa anajutia kitendo chake cha kukataa kujiunga na El- Merreikh ya Sudan alipopata nafasi hiyo. 

Winga huyo ambaye baada ya mazoezi ya jana asubuhi alipelekwa klabuni akishinikizwa azitolee ufafanuzi habari zilizotolewa juzi kuhusu hatma yake ndani ya klabu hiyo, alieleza bayana kuwa hana raha tena na soka kutokana na deni linalomkabili.

Katika mkutano uliofanyika makao makuu ya klabu hiyo, mtaa wa Twiga na Jangwani, Ngassa alieleza kuwa ameichezea Yanga kwa mapenzi, bila kulipwa chochote kufuatia mshahara wake mzima kukatwa kutokana na deni la Sh45 milioni alilokopa akiwa Simba msimu wa 2012/13.

Deni hilo, Ngassa alisema aliahidiwa na viongozi wa klabu hiyo kusaidiwa kulipa, jambo ambalo limekuwa kinyume.

Mchezaji huyo anayeichezea pia Taifa Stars aliwasili klabuni hapo saa 5.00 asubuhi, akifuatana na kocha mkuu, Hans Pluijm na meneja Hafidh Salehe, wakiwa kwenye gari dogo la klabu hiyo aina ya Hiace.

Baada ya kuwasili, Mkuu wa Idara ya Mawasiliano ya klabu hiyo, Jerry Muro, mwanasheria Frank Chacha walimpokea na kisha kuingia naye kwenye chumba cha mkutano.

Muro alianza kuzungumza kwa jazba, akiwataka waandishi wa habari kutowahoji wachezaji hadi watakapopata vibali maalumu, huku akidai vyombo vya habari vimeripoti uongo kuhusu matukio ya mchezaji huyo ndani ya klabu. 

Dakika kumi baadaye, Muro alimtaka Ngassa azungumze, ingawa mchezaji huyo alihoji aongelee kitu gani? Ndipo Muro alipomtaka aelezee safari yake ya Afrika Kusini na makato ya deni analodaiwa.

Tofauti na ilivyotarajiwa na Muro, Ngassa aliweka wazi namna uongozi wa klabu ulivyomgeuka, akijutia kitendo chake cha kukataa kujiunga na El- Merreikh ya Sudan ambako klabu za Simba na Azam zilipanga kumpeleka msimu uliopita wakati akiichezea Simba kwa mkopo kutoka Azam.

“Najutia uamuzi wangu wa kukataa kujiunga na El- Merreikh, timu iliyotaka kunipa ‘dau’ kubwa na kuamua kurudi Yanga kwa mapenzi yangu, hilo ni kosa langu siwezi, kumlaumu mtu.

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...