
Kamanda wa Jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP, Thobias Sedoyeka akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) ofisini kwake.
MTOTO wa kike mwenye umri wa miaka sita mkazi wa kitongoji cha Maweni kijiji cha Mayaha kata ya Minyughe tarafa ya Ihanja wilaya ya Ikungi mkoa wa Singida,Samaka Matawa,amefariki dunia baada ya kubakwa na kisha kunyongwa shingo.
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP,Thobias Sedoyeka, alisema tukio hilo la kusikitisha na la kinyama, limetokea majira ya jioni februari sita mwaka huu na mwili wa mtoto huyo uliokotwa na raia wema kesho yake saa 12 asubuhi ukiwa umetelekezwa hatua 150 na nyumbani kwao.
Alisema siku ya tukio, mtoto huyo Samaka alienda porini kwa lengo la kuchuma matunda pori.
0 comments:
Post a Comment