2015-02-11

Sad Neeeeewzzzzz:Moto mwingine waleta hasara Dar na Mwanza............ni hatariiiiiiiiiiiiiii



Jengo lililopo Mtaa wa Libya na Mosque likiwaka moto jijini, Dar es Salaam jana.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, alisema hakuna mtu aliyefariki wala kujeruhiwa katika tukio hilo lililotokea kwenye makutano ya Mitaa ya Libya na Mosque, Wilaya ya Ilala.

Dar es Salaam / Mwanza. Siku nne baada ya kuungua kwa nyumba iliyosababisha vifo vya watu sita wa familia moja, Dar es Salaam, moto mwingine umeteketeza sehemu ya juu ya jengo la ghorofa mbili la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lililopo katikati ya jiji.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova, alisema hakuna mtu aliyefariki wala kujeruhiwa katika tukio hilo lililotokea kwenye makutano ya Mitaa ya Libya na Mosque, Wilaya ya Ilala. 

Kamanda Kova alisema Polisi walipata taarifa jana saa 5.30 asubuhi kuwa kunguru ndio walisababisha hitilafu ya umeme na jengo hilo kushika moto na kutekekeza mali ambazo thamani yake haijafahamika.

Alisema moto huo ulioanza taratibu na kuongezeka ghafla kutokana na mitungi ya gesi iliyokuwamo kwenye jengo hilo.

Meneja wa NHC Mkoa wa Dar es Salaam, Jackson Maagi alisema jengo hilo lilikuwa na familia zaidi ya 10 na kwamba shirika hilo litahakikisha kuwa waathirika wanapatiwa nyumba za kuishi wakati utaratibu mwingine ukiendelea kufanyika.

“Tungekuwa sisi ni chanzo cha tukio hilo tungesema tuwafidie lakini kwa kuwa sisi siyo chanzo, tutawapa nyumba kwa ajili ya kujihifadhi, labda pengine chanzo halisi kitakapopatikana ndipo tutajua tufanye nini,” alisema Maagi.

Hata hivyo, mmoja wa wakazi katika jengo hilo, Ahlim Abdullah alisema jengo hilo lilikuwa na familia nne katika ghorofa ya kwanza na ofisi kadhaa katika ghorofa ya pili iliyoteketea kwa moto.

Akizungumzia chanzo cha moto huo, alisema: “Waliokuwa nje wanasema walimwona kunguru akisababisha shoti na moto kuanza kusambaa.”

Kamanda wa Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jeswald Nkongo alisema baada ya kupewa taarifa kuwa kuna moto, walituma gari la kwanza kwa ajili ya kufanya tathmini ya ukubwa wa moto ndipo walipobaini kuwa ulikuwa mkubwa na tayari ulikuwa umeshaanza kusambaa. 

Wananchi walalamika

Baadhi ya wananchi waliofika mapema katika eneo hilo walikitupia lawama Kikosi cha Zimamoto kwa kufika mapema lakini kilichelewa kuanza kuuzima moto kwa sababu ambazo hazikufahamika.

“Jengo limeanza kuungua limekuja gari likiwa na maji kidogo, wamekaa muda mrefu hawajui wafanye nini hadi tulipoanza kusaidia kuwatoa watu waliokuwa ndani.
Mwananchi

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...