
JAMAA wawili, mmoja fundi umeme, Rashid Balazi na Juma Bushiri wanadaiwa kunusurika kifo baada ya kutekwa na kusulubiwa nyumbani kwa msanii wa sinema za Kibongo, Wema Sepetu wakituhumiwa kukwapua simu ya bei mbaya ya mpambe wa mwanadada huyo, Petit Man, Amani limeichimba kwa kina.
Rashid Balazi akiwa na jeraha begani baada ya kutekwa na kupigwa.
Wakielezea mkasa huo wa kutisha uliojiri mwishoni mwa wiki iliyopita
nyumbani kwa Wema, Mtaa wa Bwawani, Kijitonyama jijini Dar,.
manusura hao walisema siku ya tukio waliitwa nyumbani kwa Wema na mdogo wake aitwaye Bite kwa ajili ya kutengeneza mota ya kusukuma maji.Walisema walifika nyumbani hapo na kuangalia mota hiyo ambapo waligundua kwamba haikuwa na tatizo bali mushkeli ilikuwa kwenye bomba la maji.
0 comments:
Post a Comment