

Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania (TFF) limesema linawashukuru mashabiki wa kanda ya ziwa kwa kuangalia mechi ya kirafiki ya kimataifa kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Malawi (The Flames) kwa ustaarabu wa hali ya juu bila kufanya vurugu.
Afisa Habari wa TFF, Baraka Kizuguto amesema ustaarabu wa mashabiki ulioonyeshwa ni wa hali ya juu katika michezo.
Vurugu zimekuwa zikitokea katika mechi kadhaa za mpira wa miguu viwanjani kwa mashabiki au wachezaji kutokubaliana na maamuzi ya marefa.
Mechi hiyo imeingiza kati ya wenyeji timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya timu ya Taifa ya Malawi (The Flames) umengiza jumla ya shilingi 73 milioni.
0 comments:
Post a Comment