Amesema baada ya kugonga kwa muda mrefu bila kufunguliwa walilazimika kubomoa mlango ambapo walikuta baba yao akiwa amening'inia juu huku tayari akiwa amekufa kwa kujinyonga ambapo mama naye alikuwa amelala kitandani huku akiwa amekwisha fariki ambapo mwili wake ukiwa na majeraha sehemu za usoni.
Amesema baada ya kupata maelezo hayo walipiga simu kituo cha Polisi ambapo walifika na kuchukua miili ya watu hao na kuipelekea hospital ya rufaa Mbeya kwa ajiri ya uchunguzi zaidi.
Kwa mujibu wa balozi huyo amedai kuwa inawezekana kuwa mwanaume huyo ambaye sasa ni marehemu alimuua mke wake kwa kumpiga na kitu kizito kichwani hadi kufa kuku yeye akijaribu kujiua kwa kutumia sumu ambayo ilishindikana na kutumia mbinu ya kujinyonga ambayo aklifanikiwa nayo.
Mmoja wa Majirani wa marehemu hao Ndugu Alex Kyabyara amesema hawakuwahi kusikia ugomvi wa aina yeyote baina ya wawili hao hivyo tukio hilo limewastaajabisha huku wakishindwa kujua nini chanzo cha mauji hayo.
Akithibisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa mbeya Ahmed Msangi amesema tukio hilo limetokea majira ya saa Nne asubuhi ambapo amedai kuwa watu hao walikuwa na ungomvi usiku wa manane hali ambayo imepelekea mauiji hayo.
Aidha kamanda msangi amekili kuwa wawili hao ambao ni mke na mume bado walikuwa ni watumishi wa shirika la umeme tanesco mkoa wa mbeya hadi umauti huo unawakuta.
Amesema bado uchunguzi zaidi unaendelea kufanyika ili kubaini chanzo cha mauiji hayo ambapo miili ya marehemu hao imehifadhiwa katika hospital ya rufaa jijini Mbeya.
0 comments:
Post a Comment