Showing posts with label UDAKU. Show all posts
Showing posts with label UDAKU. Show all posts

2015-04-10

Dimpozi: Nje nafuata fedha, mzimu wangu upo bongo


MSANII wa bongo fleva, Omary Nyembo ‘Ommy Dimpoz’, ameweka wazi kwamba huwa anakwenda katika maonyesho nchi za nje kwa sababu ya fedha, si mapenzi na nchi hizo.

Amesema hata akifika katika nchi hizo huwa anatamani kurudi mapema Tanzania, jambo ambalo huwa linamshangaza kila wakati.


Msanii huyo aliliambia MTANZANIA kwamba kinachompa kiburi cha kuendelea kufurahia nchi hii ni kutokana na amani na uhuru anaoupata, tofauti na anapokuwa katika maonyesho yake nchi za nje.

“Nimekuwa nikiandamwa na mzimu wa kukumbuka nyumbani, hivyo ndivyo ninavyoweza kusema, asikwambie mtu, nyumbani ni nyumbani, hata kama nje kuna raha kiasi gani,” alisema Ommy Dimpoz.

Ommy Dimpoz ameendelea kufanya vizuri kupitia wimbo na video yake ya ‘Wanjera’, ambao video yake imeshirikisha watu mbalimbali maarufu, akiwemo mwigizaji Wema Sepetu na mshindi wa Big Brother Africa (BBA) mwaka jana, Idriss Sultan.

KADJA: KWA MAISHA HAYA MUME WA NINI?


Staa kutoka nyumba ya kukuza vipaji Tanzania ‘THT’, Khadija Maige ‘Kadja Nito’. 

STAA kutoka nyumba ya kukuza vipaji Tanzania ‘THT’, Khadija Maige ‘Kadja Nito’, hatimaye ameamua kufunguka na kusema kuwa, kwa maisha yake ya sasa ya kimuziki haoni kama kuna umuhimu wa kufikiria masuala ya kuolewa.

Akizungumza na paparazi wetu mwishoni mwa wiki iliyopita Kadja alisema kuwa, muziki sasa ndiyo kila kitu kwake hivyo hawezi kumpa nafasi mwanaume au kuzungumzia suala la ndoa hivi sasa. 

“Naweza kuishi maisha yangu bila mwanaume, napata mshiko, nawasaidia ndugu zangu na mimi najimudu, mume wa nini maisha haya? Sasa ni muziki na mimi, mimi na muziki, mapenzi yasubiri,” alisema Kadja.
GPL

ALA KICHAPO TAKATIFU KISA MUME WA MTU


Jamila akiwa na jeraha usoni kwa tuhuma zakutembea na mume wa mtu.
 
Dada mmoja aliyefahamika kwa jina la Jamila mkazi wa Kawe jijini Dar hivi karibuni alipata kipigo cha kufa mtu akituhumiwa kuchepuka na mume wa mwanamke mmoja aitwaye Sheila.Tukio hilo lilitokea hivi karibuni ambapo ilielezwa kuwa, Sheila alitonywa na wambeya kuwa Jamila amekuwa akichepuka na mumewe na bila kuchunguza akapanga kumshikisha adabu.

“Jamila alikuwa akituhumiwa kutembea na mume wa Sheila na siku ya tukio alifuatwa baa na kupigwa hadi kutaka kutobolewa jicho,” kilidai chanzo. 

Mwandishi wetu alifanya jitihada za kuwatafuta wahusika ambapo Jamila alipopatikana alisema:
“Jamani ukweli ni kwamba mimi niliwahi kutembea na yule mume wa Sheila lakini tulishaachana sasa nimemshangaa mkewe kuja na kunipa kipigo sababu tu ya maneno ya kusikia”, alisema Jamila na kuongeza: 


                      Mwenye mume.

“Nilikwenda kufungua kesi Kituo cha Polisi Kawe lakini siku chache baadaye Sheila alikuja na kuniomba msamaha akidai kuwa alikoasea kuamini maneno ya watu bila kufanya uchunguzi. Tumesameheana na yameisha.”
GPL

Aliyekuwa Mke wa Mh Mbunge Sugu, Faiza Ally Atangaza Mtandaoni Kuwa Ana Hamu ya Kufanya Mapenzi......Kazi Kwenu Wanaume



Mrembo asiyeishiwa vituko, Faiza Ally ambaye amezaa na Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Mr Sugu’ ametoa kali baada ya kusema kuwa ana hamu ya kumpata mwanaume mwingine wa kumpa raha lakini mpaka sasa hajapata.

Kupitia Ukurasa Wake Wa Instagram, Faiza alisema tangu alipoachana na Mheshimiwa Sugu, aliona bora ajitulize lakini sasa anajiona kuna kitu anakikosa na wa kumpa kitu hicho ni mwanaume.



“Niseme tu kwamba tangu niachane na Sugu sijakutana na mwanaume mwingine, hebu ‘imagine’ ni muda gani? Sasa nimeshindwa kuvumilia, natafuta wa kunipa raha maana kuna hali flani ikinijia nakuwa kama chizi, swali ni je, nani mwanaume sahihi wa kunipa ‘zawadi’ hiyo? Hapo ndipo mtihani ulipo,” alisema Faiza.

SAJENT; ETI SASA VIMINI PEMBENI, SWALA NA YEYE!


Mwanadada muigizaji Husna Idd ‘Sajent’.
 
Kama kawa, kama dawa leo kupitia safu hii tunaye mwanadada muigizaji Husna Idd ‘Sajent’. Wengi wanataka kujua siri ya ukimya wake hivyo mwandishi wetu Hamida Hassan alimtafuta na kumpiga maswali 10 kama ifuatavyo.

Ijumaa: Husna, siku hizi huonekani kabisa kwenye anga za starehe, ni kwa nini? Au ndo tuseme umefulia?
Sajent: Sajent wa sasa si yule watu waliyemzoea, nimeamua kuishi maisha ya tofauti kabisa ndiyo maana siyo mtu wa kujiachia kivile. 

Ijumaa: Kuna habari kuwa umeolewa na msanii mwenzako Gabo na ndiyo maana hata mfumo wako wa maisha umebadilika, hilo unaliongeleaje?
Sajent: Watu wanapenda sana kuongea, acha waongee kwani siwezi kuwabadili lakini mimi na Gabo tuko karibu sana, nampenda kama msanii mwenzangu.

Ijumaa: Je, una mchumba kwa sasa? Na kama yupo, mipango ya wewe kuingia kwenye maisha ya ndoa ikoje?
Sajent: Ni kweli mchumba ninaye na Mungu akipenda nitaolewa tu.

Ijumaa: Inaweza kuwa mchumba ndiye kakubadilisha mpaka sasa huonekani na vimini kama zamani bali ni mtu wa madira kila wakati?
Sajent: Nikiri tu kwamba mchumba wangu ndiyo chanzo cha mabadiliko ya maisha yangu, amekuwa akiniongoza kumjua Mungu zaidi.

Ijumaa: Katika siku za hivi karibuni umekuwa ukionekana una mimba na hata mashosti zako walieleza kuwa, una kitumbo, hebu funguka. 

Sajent: Mh! Watu bwana, kile kitumbo ilikuwa filamu bwana. Filamu yenyewe inaitwa On Set, watu wataiona tu.
Ijumaa: Mbona inadaiwa ulikuwa nayo ukaitoa?
Sajent: Sijawahi kutoa mimba, naanzaje kufanya tukio hilo la kinyama jamani?
Ijumaa: Huyo mchumba wako anapokutembelea huwa unapenda kumpikia chakula cha aina gani?
Sajent: Mchumba wangu ni mpenzi sana wa wali samaki, hivyo akisema tu anakuja siku hiyo natulia na kumpikia ile kitu roho yake inapenda.

Ijumaa: Wewe ni muislam, kuna wakati kweli unamkumbuka mola wako?
Sajenti: Kama nilivyosema awali, sasa hivi nimebadilika na kwa kweli najitahidi kusali sala tano.
Ijumaa: Ukiwa home unapenda kufanya nini hasa?
Sajent: Ni kazi za nyumbani kama mwanamke lakini nikiwa free napenda kujisomea Quran.

Ijumaa: Ni tabia gani za mastaa wenzako ambazo zinakukera?
Sajent: Majungu, umbeya, kuchukuliana mabwana, mabifu yasiyokuwa na maana ni kati ya tabia zinazonichefua.
GPL

PENZI LA NAY, SHAMSA SIWEMA, MUME WA SHAMSA VILIO

 Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego na Shamsa Ford wakipozi kimahaba.
Penzi matata linalowanyima usingizi baadhi ya watu mjini kwa sasa kati ya mwigizaji wa sinema za Kibongo, Shamsa Ford na mkali wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ limeibua tafrani kubwa huku waliokuwa wapenzi wa mastaa hao wakijikuta wakiangua vilio kweupe, Ijumaa limesheheni.

TATIZO MAHABA NIUE
Mara baada ya wawili hao kutangazwa rasmi kuwa sasa ni mahaba niue huku picha za ushahidi zikimwagwa, aliyekuwa mwandani wa Nay, Siwema a.k.a Wemalicious na aliyekuwa mume wa Shamsa, Dickson ‘Dick’ wanadaiwa kujikuta kwenye hali mbaya kiasi cha kumwaga machozi.

TUJIUNGE NA CHANZO KWA SIWEMA
Habari kutoka kwa chanzo chetu ambacho ni mtu wa karibu wa Siwema jijini Mwanza zilidai kwamba, mara baada ya picha za wawili hao kuzagaa kwenye mitandao ya kijamii aliumia roho hasa alipomuona Shamsa akijiachia kwenye nyumba ambayo alishirikiana na Nay kuijenga.

“Yaani Siwema ameumia hadi akajikuta akiangua kilio kwa uchungu. Sikukuu ya Pasaka ilikuwa mbaya kupita kiasi kwa Siwema. “Kinachomuuma zaidi ni kwamba hata nguo zake za mtoko Shamsa anavaa ‘gym’ na kufanyia mazoezi. Jamani kuna dharau zaidi ya hiyo? “Ukweli roho inamuuma vibaya mno,” kilisema chanzo hicho kwa ombi la kutochorwa jina gazetini. 


Ney na Shamsa wakifuatilia jambo kwenye simu.

Kabla ya kuhamia kwa chanzo cha mume wa Shamsa ili kupata ubuyu kamili, gazeti hili lilimsaka Siwema ili kujua anachukuliaje jambo hilo ambapo alifunguka ya moyoni.

SIWEMA AANIKA MAZITO
Akizungumza na Ijumaa kwa njia ya simu kutoka jijini Mwanza, Siwema mwenye mvuto wa kuvunja midume shingo alianika mazito kwamba, kitendo cha Nay kumuacha na muda si mrefu kwenda kwa Shamsa ni upuuzi.

Siwema alifunguka kwamba, kinachomshangaza ni kitendo cha Shamsa kuvaa nguo zake na kufanyia mazoezi.

Mwanamama huyo alisema watu watamtukana kwa kuwa hawajui tabia ya Nay kwani hata Shamsa atamshindwa tu.

“Nilivumilia vitu vingi sana. Maumivu nayajua mimi, nyumba tuliyojenga wote, anaingia mwanamke mwingine. Namhurumia sana Shamsa kwani hajui tabia za Nay,” alifunguka mtoto mweupe, Siwema kwa uchungu.

KUMBE SIWEMA ALIJUA
Habari zilieleza kwamba, Siwema alijua muda mrefu kuwa Nay anatembea na Shamsa lakini alipomuuliza staa huyo anayetamba na Ngoma ya Akadumba alimwambia walishaachana. 


                                     Siwema.

NAY ANASEMAJE?
Akizungumzia ishu hiyo, Nay alisema kuwa yeye yupo na Shamsa na kwamba anamshangaa huyo Siwema kwani alishaachana naye.

TUJIUNGE NA CHANZO KWA MUME WA SHAMSA
Kwa mujibu wa chanzo makini, naye kama Siwema, baada ya penzi la Shamsa na Nay kuwa ndiyo habari ya mjini huku wakitupia picha za malovee mtandaoni, mume wa Shamsa, Dick alipaniki kiasi cha kutokwa machozi huku akitafuta namna ya kupooza machungu.

JB AOMBWA AOKOE JAHAZI
Habari zilidai kwamba, Dick alikimbilia kwa staa wa sinema za Kibongo, Jacob Steven ‘JB’ na kwenda kumuomba aokoe jahazi akimshitakia Shamsa kuwa ameamua kumwacha na kuamua kutembea na Nay, jambo ambalo analiona kuwa ni udhalilishaji kwani ni mkewe ambaye amezaa naye mtoto mmoja wa kiume, Terry. 


Mwanamuziki kinara wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.

Ilidaiwa kuwa, baada ya Dick kufika nyumbani kwa JB maeneo ya Ubungo-Kibangu, Dar na kumweleza hayo, mwigizaji huyo alimpigia simu Shamsa ambaye humwita Daddy na kumuuliza juu ya suala hilo ambapo alimweleza kuwa alishaachana na Dick hivyo kila mmoja ana maisha yake.

Katika hali hiyo, JB aliwataka kukaa chini na kuyamaliza kiutu uzima kuliko kuwekeana kinyongo.

SHAMSA ANASEMAJE?
Baada ya kusikia kilichopo upande wa mume wa Shamsa, gazeti hili lilimgeukia Shamsa na kumwelezea kila kitu kilichopo ambapo alionesha kumshangaa Dick kwa kuwa alishamalizana naye tangu Oktoba, mwaka jana.

“Kwanza namshangaa kwa nini anawaka wakati kila mtu ana maisha yake?“Tulishaachana tangu mwaka jana so kila mtu ana maisha yake,” alisema Shamsa ambaye kwa sasa amehamishia moyo wake kwa Nay. 


Aliyekuwa mume wa Shamsa, Dickson ‘Dick’.

DIAMOND ACHAFUA HALI YA HEWA
Wakati sakata la Shamsa na Nay likishika kasi mithili ya moto wa kifuu, mwanamuziki kinara wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amechafua hali ya hewa baada ya kutundika mtandaoni picha ya mahaba ya wapenzi hao iliyosababisha tafrani zaidi.

Diamond ambaye ni swahiba wa Nay ndiye aliyekuwa wa kwanza kuweka picha iliyomuonesha Nay ‘akibusiana’ na Shamsa kupitia ukurasa wake wa Instagram hivyo kuwapandisha hasira Siwema na Dick kwani alionekana kufurahishwa na ‘pea’ hiyo.
GPL

2015-04-09

Shamsa: Sijutii Kuachana na Mume Wangu


Staa mrembo kutoka Bongo Movies, Shamsa Ford amesema kamwe hatajutia kitendo cha kuachana na mumewe, Dickson.

Akiongea na gazeti la Amani Shamsa alisema kuwa kipindi chote wakati yupo kwenye uhusiano na mumewe huyo waliefunga naye ndo ya kimilia alikuwa akiteseka na kupata shuruba nyingi japo hakuwa tayari kuziweka hadharani. 

“Sijutii kuachana na mume wangu, nimepitia mateso mengi, sikotayari kurudi japokuwa nina motto naye” Shamsa alisema.

Kwa sasa inadaiwa Shamsa anatoka na Staa wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego ambaye naye aliachana na mchumba wake ,Siwema hivi karubuni.

KISA RIHANNA, BEYONCE NA JAY Z WAINGIA KATIKA MGOGORO

                           Beyonce na Jay Z katika pozi.

MWANAMUZIKI Beyoncé Giselle Knowles 'Beyonce' na mumewe Shawn Corey Carter 'Jay Z' wameripotiwa kuwa kwenye mgogoro tena huku mwanamuziki Rihanna akihusishwa. 

Wanandoa hao wapo kwenye mgogoro kutokana na simu ya siri ambayo Jay Z anadaiwa kuitumia kuwasiliana na Rihanna pasipo Beyonce kujua.

Wanaume wengi wana simu za siri ambazo hutumia kuwasiliana na watu wao kwa siri, ila mara nyingi wanakuwa makini kuficha simu zao katika magari yao au kazini.

Kupitia mtandao wa Rhymeswithsnitch.com: Beyonce anadaiwa kumkoromea mumewe Jay Z kwa kuwa na simu ya siri ambayo anatumia kuwasiliana na Rihanna.

Chanzo kimoja cha habari kimeliambia Jarida la Grazia kuwa: “Jay Z ana simu kadhaa ambapo mojawapo ndiyo hutumia kuwasiliana na Rihanna masuala ya kibiashara. 

“Ni kawaida anapopigiwa na mrembo huyo, Jay Z hutoka hata nje ya mkutano ili asizuruge vikao, hata akiwa kwenye meza ya chakula akipigiwa simu hutoka nje kuongea na Rihanna.”

Chanzo hicho kimeongeza kuwa Beyonce mwenye miaka 33, anajua kuwa Jay Z ana simu nyingi ila hakujua kama mojawapo ni kwa ajili ya kuongea na Rihanna na anachukia kitendo cha mumewe kuwa karibu na mwanamuziki huyo kutoka Visiwa vya Barbados.

Jay Z mwenye miaka 45, na Beyonce, hivi karibuni walisherehekea miaka saba ya ndoa yao ambapo wamefanikiwa kupata mtoto mmoja wa kike aitwaye Blue Ivy. 
GPL

Shilole Awataka Watu Wamuache Afanye Yake


Staa mrembo wa Bongo Movies na Bongo Fleva, Shilole ‘Shishi Bybee’ amewataka watu wamuache afanye kile anachokitaka kwenye maisha yake na sio kumpagia aishi vipi.

Shishi Bybee aliyasema hayo mara baada ya baadhi ya watu kumshambulia kwa maneno baada ya kuweka picha picha akiwa yupo kwenye bwawa la kuogelea.

“Yaani watu mnapenda kunipa raha sana mimi mwenywe nimejikubali na mimi nipo swimming mlitaka nivae dela??? Nioge nalo kwa hiyo tunapangiana na maisha ya nyumban pia lol! Kila mtu na life yake naombeni mniache nifanye yangu” Shishi alisema. 

Baadhi ya watu walionyeshwa kukelwa na picha hizo (hapo juu) za Shilole wakidai kuwa zinamdhalilisha kama mwanamke kwani sehemu kubwa ya mapaja yake yapo wazi.

DIAMOND AMWAGIA SIFA KEMKEM ZA BURUDANI JK!!..SOMA HAPA

Kijana huyu akihojiwa na Gadina wa Radio Efm kwenye kipindi cha Ubaoni amesema,Rais amempigia simu juzi na kumuliza saizi ya koti analovaa ili amletee zawadi kutoka Marekani.

Pili amesema wakiongeaga na Rais huwa Rais anajuwa mambo mengi ya muziki huko Amerika kuliko yeye.

Nimejiuliza hivi ni kweli Rais JK anaweza kufanya hivyo ukizingatia majukumu mazito yanayomkabili juu ya taifa na wananchi wake?

Ni kweli Rais JK anajuwa mambo ya burudani na vinavyojiri kwenye ulimwengu wa muziki kuliko Diamond?

Au kijana baada ya kupewa nafasi na Mh. Rais ameanza kujisahau na kuhisi ni saizi yake?

Mazito yaibuka mara baada ya kumbukumbu ya miaka mitatu tangu afariki Kanumba LULU, MAMA KANUMBA WAFIKA PABAYA


Marehemu Steven Kanumba enzi za uhai wake.  
HALI ni mbaya! Staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na mama wa aliyekuwa nyota wa fani hiyo, Steven Kanumba, Flora Mtegoa wamefikia pabaya baada ya mama huyo kumshushia Lulu maneno makali na ya shutuma, Amani lina taarifa.

Staa wa sinema za Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.

Habari zilizojiri ndani ya chumba cha habari cha gazeti hili zinadai kuwa, mama Kanumba amemlalamikia Lulu kwamba, amemtupa na kumtenga tofauti na zamani ambapo uhusiano wao ulikuwa kama wa mama na binti yake.

“Jamani habari nzito kwa sasa ni mama Kanumba na Lulu. Mama Kanumba anamshutumu Lulu kwa kumtenga. Anasema ni miezi mitano sasa Lulu hajafika nyumbani kwake wala kuwasiliana naye kwa simu,” kilisema chanzo kimoja.

Kikaendelea: “Hivi kesho (Jumanne iliyopita), ni Kanumba Day. Imepangwa kufanyika Dar West (Dar), inawezekana Lulu asiende au Mama Kanumba asiende. Lakini hata kama watakwenda na wakakutana, watachekeana kwa jino pembe lakini uhusiano wao si mzuri jamani.” 

Mama Kanumba akilia peke yake kaburini.

MAMA KANUMBA ATAFUTWA
Ili kupata usahihi wa madai hayo, Amani lilimsaka mama Kanumba kwa njia ya simu ambapo alipopatikana alikuwa na haya ya kusema:“Lulu si Lulu yule jamani. Lulu sasa hivi amebadilika. Awali aliniambia hatanitupa, lakini sivyo. Lulu siku hizi haji kunisalimia wala hanipigii simu.”

ANACHOAMINI YEYE
“Imefika mahali nawaza kwamba, huenda alipenda Kanumba aondoke ili yeye apate mafanikio makubwa aliyonayo sasa. Lulu amenitenga, amenitenga, amenitenga!”

MANENO YA MAMA KANUMBA KABURINI KWA KANUMBA
Juzi, Jumanne, ambayo ilikuwa siku ya kuadhimisha mwaka wa tatu tangu kifo cha staa huyo, mama huyo alishiriki kwa kwenda kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar kwa lengo la kusafisha kaburi la mtoto wake. Baada ya zoezi la kusafisha kaburi kumalizika, mama Kanumba aliongea na Amani na kuyasema haya:

“Nasikitika sana namna ambavyo Lulu amekuwa tofauti na maneno yake ya zamani kwamba atakuwa sambamba na mimi katika kuadhimisha kumbukumbu ya Kanumba. Lakini leo kama hivi, hajatokea.

“Pia nasikitishwa na kitendo cha kufanya bethidei ya mdogo wake jana (Jumatatu usiku) kule Posta wakati anajua ndiyo usiku ambao Kanumba alifariki dunia. 

Mama Kanumba akiwa na simanzi kubwa.

“Mbaya zaidi, akiulizwa na watu kwa nini sasa hivi hayupo sambamba na mimi kama zamani, anajibu majibu ambayo hayaeleweki. Kumbe maneno yake ya zamani kwamba atakuwa sambamba na mimi yalikuwa ya usaliti.

“Kwa hiyo na mimi sasa nimeamua kubaki peke yangu kama nilivyo, nitaendelea kumuenzi Kanumba mwanangu kwa sababu mimi ndiyo mama yake kwa hiyo nalia peke yangu.”

LULU ALITOA AHADI YA UONGO
Katika mazungumzo yake, mama Kanumba alikwenda mbali zaidi kwa kusema: “Kuna siku aliahidi kwamba atajengea picha ya Kanumba ikiwa ndani ya kioo na kuiweka juu ya kaburi, hajafanya hivyo. Nitafanya mwenyewe.“Labda amepuuza kwa vile anajiona anazidi kukua kisanii, ni supastaa ndiyo maana anatoa ahadi za uongo.”

ALICHOKISEMA LULU SASA
Lulu alipotafutwa juzi ili kuzungumzia malalamiko ya mama mkwe wake huyo, hakupatikana lakini wiki iliyopita alizungumza na paparazi wetu kuhusu mtazamo wa maisha yake kwa jumla ambapo alisema:“Mimi kwa sasa hivi nina mtazamo mwingine kabisa kuhusu maisha. Kwanza sidhani kama nitamwaga machozi tena kuhusu Kanumba maana nimelia sanasana.“Mtu ambaye naweza kumlilia ni mama yangu (Lucresia Karugila) na mdogo wangu. Lakini si mtu mwingine. Kwa sasa naangalia zaidi familia yangu.” 

TUJIKUMBUSHE KIDOGO
Kanumba alifariki dunia Aprili 7, 2012 kwa kuanguka katika mazingira yaliyodaiwa yalitokana na ugomvi kati yake na Lulu. Tukio hilo lilitokea nyumbani kwa Kanumba, Sinza ya Vatcan, Dar.

Baada ya kifo hicho, Lulu alikamatwa na kuwekwa mahabusu ya Segerea jijini Dar na baadaye kuachiwa kwa dhamana.

Baada ya kutoka mahabusu, yeye na mama yake walimfuata mama Kanumba na kuomba msamaha ambapo mama huyo aliupokea na kusema anamwona Lulu kama mtoto wake na yote ya nyuma yamepita. Kuanzia hapo, Lulu na mama Kanumba wamekuwa na ukaribu wa kindugu huku kila mwaka wakifanya kumbukumbu ya Kanumba pamoja.
 Katika kumbukumbu ya juzi, Lulu hakutokea na mama Kanumba alisema hajapewa taarifa yoyote. Lulu alipotafutwa kwa simu ili kumsikia anasema nini kuhusu kutotokea makaburini, hakuwa hewani!


GPL

Kimenukaaaaaaaa!!!!!!!! ROSE NDAUKA, SHETTA WADAIWA KULALA CHUMBA KIMOJA


Staa wa filamu Bongo, Rose.
 
KIMESANUKA! Mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nurdin Bilal maarufu kama Shetta anadaiwa kulala chumba kimoja na staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka katika hoteli iitwayo Kingway iliyoko mkoani Morogoro mwishoni mwa wiki iliyopita.
Chanzo makini kinachofahamu kwa undani kinachoendelea baina ya mastaa hao wawili, kimelidokeza gazeti hili kuwa tukio hilo lilijiri wakati wakielekea katika shughuli za mazishi ya muasisi wa Kundi la Tip Top Connection, Abdul Bonge aliyezikwa kijijini kwao Mkuyuni mkoani humo, ambako watu wengi maarufu walihudhuria.

“Si unajua mastaa kibao walikuwepo kwenye ule msiba, basi Rose na Shetta nao walikuwepo na wakati wa kwenda Mkuyuni, walipanda gari la Shetta hadi Morogoro mjini ambako walichukua chumba na kulala wote hadi kesho yake walipohudhuria mazishi na kurejea Dar es Salaam,” kilisema chanzo hicho.

Ili kushibisha maelezo yake, mtoa habari huyo alilitumia gazeti hili video ya wawili hao wakiwa ndani ya gari la Shetta inayomuonyesha Rose akiimba nyimbo mbalimbali za mkali huyo anayetamba na kibao chake kipya cha Shikorobo ambacho video yake imefanywa na mtayarishaji anayetamba nchini kwa sasa, Godfather wa Afrika Kusini. 


Mkali wa muziki wa kizazi kipya nchini, Nurdin Bilal maarufu kama Shetta.

Hata hivyo, haikuweza kufahamika mara moja kama uhusiano wa wawili hao ni wa siku nyingi au umeanza hivi karibuni, ingawa gazeti hili linafahamu kuwa Shetta ni mume wa mtu akiwa amezaa naye mtoto mmoja. 

Amani lilimtafuta Shetta na kufanikiwa kumpata kwa njia ya simu yake ya mkononi na aliposomewa mashtaka, kwanza alicheka na kusema kuwa ni kweli alikuwa msibani na alirejea Dar akiwa na Rose katika gari lake. 

“Ninachoweza kusema ni kuwa ni kweli nilimpa lifti Rose wakati tunaenda kwenye mazishi ya Bonge. Kulikuwa na magari mengi ambayo mtu yeyote angeweza kupata lifti na ni kweli pia tulilala Morogoro, ilikuwa ni hoteli moja lakini kila mtu alilala chumba chake, siwezi kujihusisha na hayo mambo, mimi nina familia,” alisema msanii huyo ambaye pia aliwahi kutamba na kibao cha Kerewa, alichomshirikisha Diamond.

Kwa upande wake, Rose Ndauka alipoulizwa kuhusu suala hilo, kwanza alishtuka na kuuliza zilikopatikana habari hizo kabla ya kukiri ukweli kuwa alipanda gari la Shetta na wote kulala hoteli moja mjini Morogoro, lakini kila mtu na chumba chake.

“Halafu nisingependa kuandikwa andikwa kila siku kwa mambo hayo, unajua kama mimi nina mtu wangu? Andikeni halafu tutaonana mahakamani, maana naona lengo lenu ni kuniharibia,” alisema Rose.
 

GPL

2015-04-08

DIAMOND PLATINUMZ ATAJWA KUWANIA TUZO YA 'RADIO AFRO AUSTRALIA SONG OF THE YEAR 2014’

Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz'.



 
Muonekano wa kipengele cha tuzo anachowania Diamond Platinumz.

STAA wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' ametajwa kuwania tuzo ya 'Radio AFRO Australia Song of the Year 2014' kupitia wimbo wake wa Number 1 Remix’ aliyomshirikisha staa wa Nigeria Davido.

Wasanii wengine kutoka Afrika wanaowania Tuzo hizo ni pamoja na Davido ambaye ana nyimbo nne zilizoingia, Bebe Cool ana nyimbo mbili, P-Square wana nyimbo nne, 2Face, AKA, Cassper Nyovest na Iyanya.

Tuzo hizi hufanyika kila mwaka na wasikilizaji wa Afro Radio ya Australia hupiga kura mtandanoni na msanii atakayepata kura nyingi ndiye anaibuka mshindi.

Kumpigia kura Diamond na kumfanya ashinde bonyeza hapa


GPL

Baada ya Kutemwa na Kunyang'anywa Mtoto Siwema Aendelea Kupeta, Anunua Gari Mpya Kwa hela zake Mwenyewe


Wakati Mpenzi wake wa zamani Nay wa Mitego akiwa Bize na Baby wake Mpya Shamsa Ford , Siwema Ameamua kujipoza machungu ya kuachwa na kunyang'anywa mtoto kwa kununua gari mpya.....
Ameweka Picha hiyo kwenye ukurasa wake wa Instagram na Kuandika yafuatayo:

wemalicious:
Thank u ZAMZAM MOTORS LTD.....kwakufanikisha hili...u always good to me#magari yenu yako bomba ile mbayaaa # namba ikitoka ntawambia ili msinipite barabarani!!!!



                                       wemalicious :
She cheat again......# whaaaat?

KAULI YA DIAMOND PLATNUMZ ILIYOMFANYA WEMA KUMWAGA MACHOZI JANA

IMG-20131009-WA0017
Wema Sepetu, it is alleged, is in denial after learning that her ex-boyfriend Diamond has impregnated another woman in such a short time. 
Wema posted an Instagram photo dismissing the pregnancy with a simple caption: "Mimba (pregnancy) my foot." Zari then reposted the photo expressing her disappointment. 
"Astagafululah! Sometimes we have to wish people good...this is too much Jamani hmmmmmm

Wanabongo Fleva wa 5 Anaowakubali Wema Sepetu, Diamond Namba Moja!


Staa mrembo kutoka Bongo Movies, Wema Sepetu pamoja na kutengena na mpenzi wake Nassib Abdul ‘Diamond’ lakini alipoamua kutaja wasanii wanaofanya vizuri katika muziki wa Bongo Fleva mtaliki wake huyo kampa namba moja katika wasanii watano ambao yeye anaona wanafanya vizuri katika muziki. 

“Muziki umeshika kasi na kuna wasanii ambao wanafanya vinzuri kuliko wengine, kwangu Top 5 yangu 1 Nassib, wa pili ni Ashley, Ali kiba, Barnaba na wa tano ni mirrow hawa ni wasanii wazuri wapo level za kimataifa,”anasema Wema. 

Aidha Wema amesema kwa upande wa wasanii wa kike anampenda sana mwimbaji Vanessa Mdee kwani anaimba na kucheza katika kiwango cha juu na kumfanya awe ni mpenzi wa kazi za msanii huyo, pia anataka watu wasimuelewe vibaya ni kwa mujibu wa mapenzi yake na maono yake.

FC

Rose Ndauka: Pengo la Kanumba bado lipo

 
NYOTA wa kike wa filamu nchini, Rose Ndauka, amesema pengo la msanii mwenzake, marehemu Steven Kanumba, litaendelea kuwepo kutokana na mchango wake mkubwa alioutoa kwenye tasnia hiyo.

Wakati jana ikiwa ni kumbukumbu ya miaka mitatu tangu Kanumba afariki dunia, Rose alizungumza na MTANZANIA na kusema kwamba msanii huyo aliikuza tasnia hiyo kwa kutumia wasanii chipukizi, akishirikiana na nyota wengine wenye majina makubwa.

“Pengo la Kanumba litaendelea kuwepo na tutazidi kumkumbuka, kwani alipenda kuona kila msanii chipukizi anafanya vizuri, lakini kwa sasa tasnia hii inayumba kwa kukosa ushirikiano na ushindi ambao ulikuwa ukiletwa na mwenzetu,” alisema Rose, akiongeza kwamba tangu Kanumba afariki hakuna mabadiliko yoyote yaliyotokea.

Zari awatuliza wabaya wake............ni balaaaaaaaaaaaa

 
 MPENZI wa msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Nassib Abdul ‘Dimond’, Zarinah Hassab ‘Zari The Boss Lady’, amewakata mdomo waliokuwa wakimbeza kuwa hana ujauzito kwa kuweka picha kwenye mtandao wake wa Instagram akionyesha ‘kitumbo’ chake.

Watu mbalimbali walikuwa wakionyesha kutokuamini ujauzito wa mrembo huyo, huku wengine wakidai kuwa ni ya kutengeneza.

Msanii huyo wa Uganda, Zari, ambaye amekuwa kimya, juzi aliamua kuweka picha zake mbili kwenye mtandao wake wa Instagram, ambazo zilimuonyesha akiwa amelala katika kiti huku ‘kitumbo’ chake kikitokelezea.

Ingawa hakuweka ujumbe wowote kwenye picha hizo, lakini imeonekana kama alikuwa anajibu mapigo kwa wabaya wake.

Baby Madaha ataka ubunifu kwenye kazi


MSANII wa filamu pamoja na muziki, Baby Madaha, amesema sanaa ya sasa inatakiwa kuwa na ubunifu, ili kuweza kufikia katika kiwango cha juu.

Akizungumza na MTANZANIA, Madaha alisema asilimia kubwa ya wasanii wanakuwa hawana ubunifu katika sanaa, kitu ambacho kinawafanya washindwe kufanya vizuri.

“Mashabiki wetu wameendelea sana na wanajua kitu bora na magumashi. Hivyo kwa sasa tunatakiwa tuendeleze ubunifu ili kuweza kuwagusa mashabiki wetu na hata kuwafikia wenzetu wa nje,” alisema.

“Sanaa ya sasa siyo ya kuingia kichwa kichwa, ndiyo maana baadhi ya wenzetu wanaingia kwenye tasnia kupitia sehemu kama THT na Bongo Star Search ili kujipika vizuri.”

Umelisikia Sharti la MAKAHABA ( Machangudoa) Wa Nigeria Walilolitoa Kwa Rais Mpya??......Wako Tayari Kugawa Uroda Bure Kwa Siku 3 Iwapo.....!


Waswahili wanasema ahadi ni deni.. akina dada ambao wanafanya biashara ya kuuza miili yao Nigeria nao wanaahidi kutimiza ahadi yao ya kutoa huduma bure kwa wateja wao nchi nzima.

Chama cha wasichana hao ambao wanafanya biashara hiyo Nigeria waliahidi kwamba wako tayari kutoa huduma bure kwa mtu yoyote iwapo Rais Buhari atashinda Uchaguzi huo..

Kwa kuwa tayari Buhari kashinda wamesema watatoa huduma hiyo kwa siku tatu bure iwapo Rais huyo ataruhusu biashara hiyo kuwa halali kabisa kama ilivyo biashara nyingine.

Chama hicho ambacho kinaitwa NANP kimesema iwapo biashara hiyo ikihalalishwa itasaidia waweze kufanya biashara yao kwenye mazingira ya usalama zaidi hata wa afya zao.. NANP walikuwa na imani kwamba Rais Buhari ataruhusu biashara hiyo japo mpaka sasa hajatoa taarifa yoyote.

Iliwahi kusikika pia kutoka Kenya ambapo wanawake wanaofanya biashara hiyo waliandamana mpaka kwa Mwanasheria Mkuu kutaka biashara yao ihalalishwe, watambulike na walipe kodi kama wafanyabiashara wengine tu.
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...