2015-02-10

Azam kuitoa Yanga kileleni..........ni hatariiiiiiiiiiiii!!!!!!!!



                                    Wachezaji wa Azam

Mabingwa wa Tanzania Bara, Azam itacheza na Mtibwa Sugar Jumatano hii katika jitihada za kuiondoa kileleni mwa ligi, klabu ya Yanga.

Azam, baada ya kutoka sare ya 2-2 na Polisi Morogoro hivi karibuni, inahitaji pointi tatu muhimu ili kufikisha pointi 25, kuwa kileleni sawa na Yanga.

Yanga ilifanikiwa kuwa kileleni mwa ligi kuu ya timu 14 baada ya kuifunga Mtibwa Sugar 2-0 katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam juma lililopita.

Hata hivyo, Azam, ambao ni wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika, wasitegemee ushindi mwepesi kwani wapinzani wao, Mtibwa Sukari wamesema hawapo tayari kupoteza mechi mbili kwa mfululizo katika jitihada zao za kutafuta ubingwa kwa mara ya kwanza.

0 comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...