
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva akisalimia na Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye kwenye mkutano wa pamoja na viongozi wa vyama vya siasa wa kujadili maboresho ya uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa, Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuvaakisalimiana na Katibu wa NEC Oganaizeshen CCM, Dk.Mohamed Seif Khatibu.
Wadau mbali mbali wa vyama vya siasa 


Mwenyekiti wa Chama cha United Demoratic (UDP), John Cheyo akipitia ratiba wakati wa mkutano huo. 

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva (kushoto), akizungumza wakati wa mkutano wa pamoja na viongozi wa vyama vya siasa wa kujadili maboresho ya uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa, Dar es Salaam. 

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe (kushoto), akiteta na Katibu Mkuu wa ACT -Tanzania, Samson Mwigamba wakati wa mapumziko. Viongozi hao waliwahi tibuana na kusababisha Mwigamba kuhamia chama hicho kipya kutoka Chadema. 

Katibu wa Itikadi na
Uenezi wa CCM, Nape Nnauye (kushoto) akifurahia jambo na Mwenyekiti wa
NCCR-Mageuzi, James Mbatia (kulia) pamoja na Katibu Mkuu wa Chadema,
Willblod Slaa wakati wa mapumziko katika mkutano wa Tume ya Taifa ya
Uchaguzi na Viongozi wa vyama vya siasa wa kujadili maboresho ya
uandikishaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura Kura ya Maoni ya Katiba
Inayopendekezwa, Dar es Salaam

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi akisisitiza jambo wakati wa mkutano wa Tume ya Uchaguzi na wadau wa Vyama Vya Siasa. Msajiri wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akizungumza wakati wa mkutano huo ambapo aliwaambia Tume ya Uchaguzi inabidi iwe na utaratibu wa kujibu maswali ama hoja za wananchi kwa wakati ili kuondoa wasiwasi wa kuelewa. 

Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe akichangia hoja kwenye mkutano huo. 

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye (kulia) akifurahia jambo na Katibu Mkuu wa Chadema Dk.Wilbrod Slaa.
0 comments:
Post a Comment